Thursday, April 23, 2015

USAFI WA MAZINGIRA KATIKA BIASHARA


Usafi ni swala linalohusu nyumbani au mwili wako pekee bali pia ni muhimu kwa mazingira yanayotuzunguka eneo la biashara. Unapoendesha biashara mfano chakula huku eneo ambalo unafanyia biashara likiwa limezungukwa na maji machafu au uchafu mwingine licha ya hatari ya kuleta magojwa kwako na kwa  wateja ni rahisi sana pia kukimbiwa na watejsa.uchafu hukaribisha nzi wanaosambaza magonjwa, kama vile kipindupindu na magojwa mengine ya tumbo.
Kutokana na uchafu kutokuwa na faida wafanya biashara hawana budi kuhakikisha wanatunza na kusafisha mazingira ya biashara zao kila siku.kuna  maeneo ambayo watumiaji wa bidhaa zinazozalishwa katika mazingira machafu hawana jinsi ya kupata huduma ya chakulahivyo kulazimika kula kilichopo katika hali yeyote.
Hakuna huruma kwa mtu mchafu Zaidi ya kumkimbia na kutafuta eneo jingine la kulana kununua bidhaa nyingine mahali pasafi penye hewa nzuri, mwanga wa kutosha na nafasi, ndio mteja mwenye kupenda kufahamu dhamani ya fedha anayolipa kwa ajili ya huduma atapenda kufika kupata huduma..
Kutokana na maelezo  yanayotolewa na wataalamu wa maswala ya usafi katika biashara wakiwemo wanaoendesha mtandao wa usafi katika biashara ni jambo la lazima.


mazingira ya kufanyia biashara yakionekana katika hali ya usafi
Hata hivyo wanasema, baadhi ya wafanyabiashra wanachukulia suala la usafi katika biashara kuwa jambo la hilari . inaelezwa kuwa wanafanya hivyo wakiamini kwamba kuweka mazingira ya biashara zao kwaenye hali ni kupenda kwa mfanya biashra husika.
Kutokana na kinachoelezwa na wataalamu katika mitandao hiyo ni vizuri wafanyabiashara wakajiuliza, usafi ni kwa faida ya nani? Nadharia ni kwamba hakuna anayeaweza  kwenda kununua bidhaa Fulani katika duka  flani lililoko katika eneo chafu halafu akakaa kimya.wengi huzungumza walichikiona kwa marafiki na famialia kuonesha kuwa wamekerwa.
Kuzungumza huko kunaonyesha kukerwa , jambo ambalo kuna mtandao unasema ndio maana wanayasema yote mabaya kwa wengine hivyo kufanya biashara husika ishuke umaarufu na kukosa wateja .mteja mmoja akiona jambo baya linlohusu usafi ni lazima ataifikiria afya yake.
Anapokuwa akilalamika mwingine naye anasikia na kumweleza jirani yake.kusambaa huko kwa taarifa kunaweza kumsababishia mwenye biashara iliyozingirwa na usafu au inayotelekezwa na wahudumu wachafu hasara.
Wafanyabiashara wanaoelewa umuhimu wa usafi wanataka wenzao waelewe umuhimu wa usafi wanataka wenzao waelewe kuwa wateja wanao wahudumia kwa kuwauzia bidhaa au huduma mbalimbali wanaelewa thamani na umuhimu wa usafi wa mazingira yanayozunguka biashara.

No comments:

Post a Comment